Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) 2025 inaielekeza Serikali kuendelea na ujenzi wa miundombinu ya Mabasi Yaendayo Haraka (BRT) ili kuwezesha wananchi kufika kwa urahisi na kwa haraka kwenye makazi, biashara na huduma muhimu. Nina furaha kuona tunatekeleza ahadi hiyo ambapo leo nimezindua Awamu ya Pili ya BRT katika barabara za Kilwa, Chang’ombe, Sokoine na Kawawa jijini Dar es Salaam.
Mradi huu umeanza kuleta matokeo chanya kwa kupunguza muda wa safari kutoka zaidi ya saa moja hadi takribani dakika 30, kupunguza msongamano wa abiria na magari, pamoja na kuongeza fursa za ajira, hususan kwa vijana. Azma yetu ni kukamilisha awamu zilizobaki ili wananchi wengi zaidi wanufaike na huduma hii.
Ili kuhakikisha miradi hii inakuwa na manufaa ya kudumu, nimetoa maelekezo yafuatayo:
1. Wizara Ujenzi, TAMISEMI na mamlaka zinazohusika ziimarishe usimamizi wa miradi yote ili ikamilike kwa wakati na itoe huduma kwa wananchi.
2. Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) uongeze mabasi kulingana na mahitaji halisi ya abiria.
3. Wananchi watunze miundombinu inayojengwa ili idumu.
4. Wizara ya Ardhi na mamlaka za serikali za mitaa zitenge mapema na kulinda maeneo yatakayojengwa miundombinu.
2K Followers 626 FollowingPartnering with governments, businesses, and organizations to solve complex challenges through strategy, technology, and innovation